RAIS TRUMP AFUNGUKA BAADA YA KUNUSURIKA KUUAWA

Date:

Share post:

WASHINGTON DC, Marekani

RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema hakuwa na hofu wakati wa shambulizi la risasi katika hafla ya waandishi wa habari wa Ikulu aliyohudhuria mjini Washington DC.

Mwanaume mwenye umri wa miaka 31 aliyefahamika kwa jina la Cole Tomas Allen, ndiye aliyefyatua risasi jirani na eneo la ulinzi wa Rais Trump.

Baada ya kusikika kwa milio ya risasi, walinzi walilazimika kumkimbiza na kumficha Rais Trump kwenye chumba maalumu.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Todd Blanche, amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa alilenga kuwadhuru viongozi wa utawala wa Rais Trump.

Akihojiwa baada ya tukio hilo, Rais Trump amesema: “Sikuogopa. Nayaelewa maisha. Tunaishi kwenye dunia yenye wendawazimu mwingi.”

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

MEGAN AACHANA NA MPENZI WAKE KISA ‘KUCHEPUKA’

LOS ANGELES, Marekani BIBIYE mwenye jina kubwa katika soko la muziki wa Hip hop nchini Marekani, Megan thee stallion,...

SERIKALI YAWEKA WAZI MKAKATI WA KUIFANYA SEKTA YA MADINI KUWA MHIMILI WA UCHUMI

Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma leo Aprili 27, 2026,...

KINDA AJAX AZIGONGANISHA ARSENAL, CHELSEA

LONDON, Uingereza KLABU za Arsenal na Chelsea zimeingia kwenye vita ya kuiwania saini ya staa wa Ajax ya Uholanzi,...

MABORESHO YA UWANJA WA BENJAMINI MKAPA YAANZA RASMI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson...