MEGAN AACHANA NA MPENZI WAKE KISA ‘KUCHEPUKA’

Date:

Share post:

LOS ANGELES, Marekani

BIBIYE mwenye jina kubwa katika soko la muziki wa Hip hop nchini Marekani, Megan thee stallion, ametangaza kuachana na mpenzi wake, Klay Alexander Thompson.

Megan ametumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram kutangaza taarifa hiyo, pia akisema chanzo ni mshikaji huyo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake wengine.

Alexander Thompson ni mmoja ya mastaa wa Ligi Kuu ya Kikapu ya Marekani (NBA) akiwa na klabu ya Dallas Mavericks.

Katika hatua nyingine, Megan ambaye pia ni mwigizaji wa filamu amesema kwa sasa anahitaji kuwa ‘singo’ ili kuilinda afya yake ya akili.

Kwa upande wake, Alexander Thompson amedai kuwa mrembo huyo ndiye aliyekuwa wa kwanza ‘kuchepuka’ na ndipo alipoamua kulipiza kisasi.

“Alikuwa wa kwanza kunisaliti, nikalipiza kisasi. Nimeumia kwa sababu nilitumia zaidi ya Dola milioni nne kwa ajili yake. Sitorudia,” amesema.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SERIKALI YAWEKA WAZI MKAKATI WA KUIFANYA SEKTA YA MADINI KUWA MHIMILI WA UCHUMI

Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma leo Aprili 27, 2026,...

KINDA AJAX AZIGONGANISHA ARSENAL, CHELSEA

LONDON, Uingereza KLABU za Arsenal na Chelsea zimeingia kwenye vita ya kuiwania saini ya staa wa Ajax ya Uholanzi,...

MABORESHO YA UWANJA WA BENJAMINI MKAPA YAANZA RASMI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson...

ANTONIO CONTE ATAJWA KURUDI CHELSEA

LONDON, Uingereza HUENDA kocha raia wa Italia, Antonio Conte, akarejea kuliongoza benchi la ufundi la Chelsea lililoachwa wazi na...