BAYEN WAGOMA KUMBAKIZA JACKSON

Date:

Share post:

MUNICH, Ujerumani

BAYERN Munich wamethibitisha kuwa hawatomsajili moja kwa moja mshambuliaji wanayemtumia kwa mkopo kutoka Chelsea, Nicolas Jackson.

Jackson alisajiliwa kwa mkopo mwaka jana na mkataba wake ulikuwa na kipengele kinachoiruhusu Bayern kumsajili kwa Pauni milioni 56.2.

Nyota huyo amekuwa na mchango mkubwa kwa Bayern akishirikiana na Harry Kane, ambapo ameshafunga mabao matano na ‘asisti’ mbili katika mechi saba zilizopita.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Michezo wa Bayern, Max Eberl, amefichua kuwa Jackson atarejea Chelsea mwishoni mwa msimu huu.

“Hatutotumia kipengele cha kumbakiza Nicolas Jackson,” amesema Eberl katika mahojiano yake na kituo cha televisheni cha ZDF.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

MEGAN AACHANA NA MPENZI WAKE KISA ‘KUCHEPUKA’

LOS ANGELES, Marekani BIBIYE mwenye jina kubwa katika soko la muziki wa Hip hop nchini Marekani, Megan thee stallion,...

SERIKALI YAWEKA WAZI MKAKATI WA KUIFANYA SEKTA YA MADINI KUWA MHIMILI WA UCHUMI

Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma leo Aprili 27, 2026,...

KINDA AJAX AZIGONGANISHA ARSENAL, CHELSEA

LONDON, Uingereza KLABU za Arsenal na Chelsea zimeingia kwenye vita ya kuiwania saini ya staa wa Ajax ya Uholanzi,...

MABORESHO YA UWANJA WA BENJAMINI MKAPA YAANZA RASMI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson...