SITA MBARONI KWA TUHUMA ZA MAUAJI JIJINI ARUSHA

Date:

Share post:

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha linawashikilia watu sita kwa tuhuma za mauaji ya askari polisi, Roland Mollel, yaliyotokea usiku wa Aprili 15 katika eneo la Mlimani, Kata ya Muriet jijini Arusha.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo, tukio hilo lilitokea wakati askari huyo alipokuwa akifanya shughuli zake binafsi baada ya kazi.

Aidha amesema kabla ya tukio hilo kulizuka taharuki miongoni mwa wananchi kufuatia taarifa za kuwepo kwa watu waliodaiwa kuwa wezi katika eneo hilo.

Katika mkanganyiko huo, marehemu akiwa amepanda pikipiki pamoja na mtu mwingine anayedaiwa kuwa dereva wa bodaboda, walishambuliwa na kundi la watu waliokuwa wakiwafukuza kwa tuhuma hizo.

Polisi wamesema wanaendelea na msako wa kuwatafuta watuhumiwa wengine waliohusika na tukio hilo huku uchunguzi ukiendelea kukamilishwa.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi kuepuka kujichukulia sheria mkononi, huku likisisitiza kuwa vitendo hivyo ni kinyume cha sheria na vinaweza kusababisha madhara kwa watu wasio na hatia.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa...