LONDON, Uingereza
UONGOZI wa Newcastle United unaangalia uwezekano wa kumrejesha Ligi Kuu ya England kocha wa zamani wa klabu za Chelsea na Manchester United, Jose Mourinho.
Kocha wa sasa, Eddie Howe, anakabiliwa na presha kubwa kutokana na mwenendo usioridhisha wa timu hiyo, licha ya usajili wa bei kubwa aliofanya.
Ukiacha jina la Mourinho anayeinoa Benfica ya Ureno, kocha mwingine anayehusishwa na Newcastle ni Roberto Mancini aliyewahi kufanya kazi Manchester City.
Wakati huu Howe akitajwa kukalia kuti kavu, Newcastle pia inatarajiwa kupoteza baadhi ya wachezaji wake muhimu mwishoni mwa msimu huu.
Miongoni mwa nyota hao ni Sandro Tonali, Tino Livramento na Anthony Gordon anayehusishwa na klabu za Bayern Munich na Arsenal.
Imeandaliwa na Hassan Mwasha






