SENESI SASA AINGIA RADA ZA LIVERPOOL

Date:

Share post:

MERSEYSIDE, Uingereza

KLABU ya Liverpool imeanza rasmi mbio za kunasa saini ya beki wa Bournemouth, Marcos Senesi.

Taarifa za Senesi kuondoka Bournemouth zimeongezeka tangu kocha Andoni Iraola aliposema ataondoka mwishoni mwa msimu huu.

Licha ya Bournemouth kuhaha kumbakiza, ripoti zinaeleza kuwa Senesi hana mpango wa kusaini mkataba mpya klabuni hapo.

Liverpool inahitaji mlinzi wa kati wa kusaidiana na Virgil van Dijk baada ya kupanda na kushuka kwa viwango vya Ibrahima Konate na Giovanni Leoni.

Mbali ya Liverpool, klabu zingine zilizoripotiwa kumtolea macho Senesi ni Chelsea, Manchester United, Juventus na AS Roma.

Imeandaliwa na Hassan Mwacha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa...