ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Date:

Share post:

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran Hezbollah nchini Lebanon licha ya shinikizo la kimataifa kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano.

Netanyahu amesema majeshi ya Israel yako karibu kuudhibiti mji wa kusini mwa Lebanon wa Bint Jbeil ambao anautaja kuwa ngome ya Hezbollah.

Baraza la Mawaziri la Israel linaripotiwa kukutana kujadili uwezekano wa kufikiwa makubaliano ya kusitisha mapigano lakini bado hakujatangazwa uamuzi wao kuhusiana na hilo.Iran inasisitiza kuwa Lebanon sharti ijumuishwe katika makubaliano yoyote ya kuvimaliza vita vya Mashariki ya Kati.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

SENESI SASA AINGIA RADA ZA LIVERPOOL

MERSEYSIDE, Uingereza KLABU ya Liverpool imeanza rasmi mbio za kunasa saini ya beki wa Bournemouth, Marcos Senesi. Taarifa za Senesi...