MILIONI 18 ZAMLIZA MBUNGE WA CCM

Date:

Share post:

MACHI 5, 2018
Mbunge Tweve
IRINGA 
Mbunge wa Viti Maalumu wa Mkoa wa Iringa, Rose Tweve, leo amelia machozi hadharani baada ya kupewa shuilingi milioni 18 kwa ajili ya mradi ya maendeleo ya akina mama.
Tweve amepewa fedha hizo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Salimu Asas mbele ya wajumbe wa Bara za Wanawake (UWT) la CCM, Wilaya ya Mufindi ukiwa ni mchango wake kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya akina mama.
Asas aliamua kutoa fedha hizo kumuunga mkono Tweve ambaye aliyetoa sh. 600,000 kwa kata 17 za wilaya hiyo kwa ajili ya kuinua uchumi wa wananchi.
Imeelezwa kuwa lengo Tweve ni kutoa Sh. Milioni 60 kwa kata zote za Mkoa wa  Iringa.
Assas baada ya kutoa kiasi hicho cha fedha alisema amefurahishwa na mkakati wa Tweve wa kuwafikia wananchi wa kipato cha chini wanaostahili kuinuliwa kiuchumi.
Tweve baada ya kupokea fedha hizo huku machozi yakimbubujika alisema anajisikia furaha na amani kuona watu wanathamini mchango wake katika jamii na kumuunga mkono.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

LONDON, Uingereza BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...