LONDON, Uingereza
KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi wake waandae kitita cha Pauni milioni 43.
Beki huyo wa kushoto amewahi pia kuhusishwa na klabu kubwa mbili za England, Manchester City na Manchester United.
Nyota huyo raia wa Hispania, ni ‘panga pangua’ katika kikosi cha kwanza cha Barcelona chini ya kocha Hansi Flick.
Hata hivyo, majeraha ya misuli yaliyomkumba mara mbili hivi karibuni yalisababisha akose mechi 10.
Kukosekana kwake kumempa nafasi kubwa Joao Cancelo, ambaye Barcelona wanaangalia uwezekano wa kumsajili moja kwa moja baada ya mkopo wake kuisha mwishoni mwa msimu huu.






