LONDON, Uingereza
RIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko la asilimia 2.1 ukilinganisha na takwimu za mwaka 2024.
Pia, kwa mujibu wa ripoti hiyo, ni ongezeko la wahamiaji zaidi ya milioni 24, ukilinganisha na takwimu za mwaka 2010.
Ripoti ya Kituo cha Tafiti na Uchambuzi wa masuala ya Uhamiaji (Centre for Research and Analysis on Migration) imeitaja Ujerumani kuwa kinara wa kupokea wahamiaji barani Ulaya.
Taasisi hiyo imeeleza kuwa Ujerumani ina wahamiaji takribani milioni 18, ongezeko la asilimia takribani 70, ukilinganisha na mwaka 2010.
Kwamba asilimia 21.2 ya watu nchini Ujerumani ni wahamiaji, huku asilimia 72 kati yao wakiwa na umri wa kufanya kazi.






