RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

Date:

Share post:

TAIPEI, Taiwan
RAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha uamuzi wake huo.

Mataifa hayo yamekuwa kwenye mvutano wa miaka mingi, huku kukiwapo kwa tishio la China kuivamia kijeshi Taiwan.

Ching-te amesema mamlaka za China zimesababisha kukwama kwa safari yake kutokana na kuweka shinikizo kwa baadhi ya nchi kuzuia ndege yake kutumia anga zake.

Sshelisheli, Mauritius na Madagascar zimeripotiwa kuinyima kibali ndege ya kiongozi huyo kupita kwenye mipaka yake ya anga.

Hatua hiyo imetokana na China kuzipa vitishio vya kuziwekewa vikwazo vya kiuchumi endapo zingeruhusu ndege ya Rais Ching-te kutumia anga zake.

Aidha, China imekanusha taarifa hizo, ikisema haijaweka vitisho vya aina hiyo, licha ya kupongeza hatua iliyochukuliwa na mataifa hayo ya Afrika.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU ZIARA YA PAPA LEO BARANI AFRIKA

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, yuko barani Afrika kwa ziara ya siku 10 katika mataifa...

MATESO WANAYOPITIA WATOTO KATIKA MACHAFUKO YA SUDAN

DARFUR, Sudan "HALI ya watoto nchini Sudan inazidi kuwa mbaya kila baada ya saa moja." Hiyo ni kauli ya...

IRAN: TUKO TAYARI KWA VITA MAZUNGUMZO YAKISHINDIKANA

TEHRAN, IranSPIKA wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema nchi yake itakuwa tayari kwa mbinu mpya za...

RAIS WA BRAZIL AMVAA TRUMP, AITAKA AFRIKA KUSINI KUMPUUZA

BERLIN, Ujerumani RAIS wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva, amesema Donald Trump hana mamlaka ya kumzuia Cyril Ramaphosa...