RAIS WA BRAZIL AMVAA TRUMP, AITAKA AFRIKA KUSINI KUMPUUZA

Date:

Share post:

BERLIN, Ujerumani

RAIS wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva, amesema Donald Trump hana mamlaka ya kumzuia Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini kushiriki Mkutano wa G20.

Akizungumza mjini Hannover, Ujerumani jana Aprili 20, 2026, Da Silva amemtaka Rais Ramaphosa kupuuzia kauli za Trump, na badala yake kuhudhuria Mkutano huo.

“Nimemwambia Ramaphosa kwamba anapaswa kuhudhuria Mkutano wa G20. Anapaswa kuwepo. Hawezi kukosekana eti kwa sababu Trump ameamua,” amesema.

Inafahamika kuwa uhusiano wa Afrika Kusini na uongozi wa Rais Trump umezorota kwa miaka ya hivi karibuni.

Kutokana na madai yake kuwa Serikali ya Afrika Kusini imekuwa ikisimamia mauaji ya watu weupe nchini humo, Trump amechukua hatua kadhaa dhidi ya uongozi wa Rais Ramaphosa.

Mbali ya kuzuia misaada ya kifedha, pia ametoa nafasi kwa watu weupe wa Afrika Kusini kwenda kuishi Marekani endapo wanahisi kudhulumiwa haki zao katika Taifa hilo la Afrika.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...

USIYOYAJUA KUHUSU ZIARA YA PAPA LEO BARANI AFRIKA

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, yuko barani Afrika kwa ziara ya siku 10 katika mataifa...

MATESO WANAYOPITIA WATOTO KATIKA MACHAFUKO YA SUDAN

DARFUR, Sudan "HALI ya watoto nchini Sudan inazidi kuwa mbaya kila baada ya saa moja." Hiyo ni kauli ya...

IRAN: TUKO TAYARI KWA VITA MAZUNGUMZO YAKISHINDIKANA

TEHRAN, IranSPIKA wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema nchi yake itakuwa tayari kwa mbinu mpya za...