BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza

BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar Sarr.

Tottenham ilimsajili Sarr mwaka 2021, kisha ikampeleka kwa mkopo Mainz, kabla ya kumrudisha na kuwa mchezaji tegemeo tangu mwaka 2023.

Kwa miaka mitatu, nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 ameshacheza mechi 135 na kufunga mabao 11.

Kwa mujibu wa mtandao wa Football Insider, Bayern, Fenerbahce na Real Madrid zinapigana vikumbo kuinasa saini yake.

Kwa sasa, bado mchezaji huyo ana mkataba na Tottenham, ambao unatarajiwa kufikia ukomo mwaka 2030.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...

USIYOYAJUA KUHUSU ZIARA YA PAPA LEO BARANI AFRIKA

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, yuko barani Afrika kwa ziara ya siku 10 katika mataifa...