Nusu kaputi = Nusu kuua

Date:

Share post:

MACHI 5, 2018
Dk. Mpoki
DAR ES SALAAM
Maneno nusu kaputi yanalotumiwa na watalaamu wa dawa za usingizi yanamaanisha kumuua mtu nusu na nusu nyingine anabaki akiwa hai.
Tafasili ya maneno hiyo imetoleana na Katibu Mkuu wa  Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubisya alipokuwa akifungua mafunzo ya awamu ya tatu kwa wataalamu wa dawa za usingizi jijini Dar es  Salaam leo.
Dk Mpoki alisema neno hilo ni baya kwa sababu linawaogopessha wagonjwa wanaotakiwa kufanya upasuaji ambao ni lazima wapatiwe dawa hiyo ya usingizi.
Aliwashauri watalaamu hao kuwa, badala ya kutumia maneno nusu kaputi watumie maneno tiba ya dawa za usingizi.
Alisema msingi wa kuwataka wasitumie maneno nusu kaputi na badala yake watumie maneno tiba ya dawa ya usingizi ni kwa sababu mtu anapopewa dawa ya usingizi huwa analala na baadaye huamka lakini hauawi nusu na nusu nyingine kubaki akiwa hai.
 “Dawa ya kulaza wagonjwa au dawa ya usingizi inatolewa ili mgonjwa anapofanyiwa upasuaji asisikie maumivu anapokatwa mwilini, hivyo siyo sahihi kusema mgonjwa kauawa nusu na nusu kaachwa akiwa hai” alisema Dk. Mpoki..

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

LONDON, Uingereza BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...