CHADEMA YALIA KUCHEZEWA RAFU

Date:

Share post:

Tumaini Makene

 

NA MWANDISHI WETU

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeeleza masikitiko yake dhidi ya watu wanaokichafua katika mitandao ya kijamii. 

 Akizungumza na Tanzania PANORAMA Blog, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema, Tumaini Makene alisema watu wenye nia ovu na chama hicho wamekuwa wakisambaza ujumbe wa kupotosha katika mitandao ya kijamii kwa lengo la kuwatisha au kuibua taharuki kwa wanachama, wafuasi na mashabiki wa chama.

Alisema barua iliyosambaa jana mitandaoni inayoonyesha kuandikwa na kusainiwa naye, Septemba 5, 2020 ni kielelezo cha matendo machafu kinachofanyiwa Chadema na watu wasiokitakia mema.

Freeman Mbowe


 “Barua ya uongo yenye ujinga kama hiyo wanaweza kuamini tu waliyoitengeneza kujifurahisha kwa mahitaji yao wenyewe kaka,” alisema Makene. 

Barua hiyo yenye kichwa cha maneno ‘chama cha demokrasia na maendeleo, taarifa kwa viongozi wote wa kanda’ inaonyesha kusainiwa na Makene na inasomeka;

“Kichwa cha habari tajwa chahusika. Rejeeni kikao cha tarehe 25.08.2020 ambacho kilikuwa ni kikao kazi na tathimini ya hali ya fedha kuelekea uchaguzi mkuu 2020.

 “Naomba kuwajulisheni rasmi kuwa tutawezesha kwa asilimia 25 tu na inayosalia tumieni mfumo wa harambee licha ya ugumu uliopo hasa ukizingatia wafadhili wote wa ndani kuhofu kutuchangia kwa sababu za kisiasa.

 “Pia tuna taarifa kuwa yapo majimbo ambayo wagombea wetu wameishaingiwa na wasiwasi wa ushindi na tayari dhamira zao zinatupa mashaka. Hili halikubaliki na tayari tumeishawatumia timu ya kuchunguza ili kujitathimini kabla ya awamu ya kwanza ya kampeni kwa mujibu wa vikao vyao vya ndani. Lazima mapambano yaendelee.

 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

GUARDIOLA AMPONZA KOCHA WA BURNLEY

LONDON, Uingereza KOCHA wa Burnley, Scott Parker, amekalia kuti kavu baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na Manchester...

BERNARDO AWEKA REKODI MPYA MAN CITY

MANCHESTER, Uingereza KATIKA ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley, kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, ameweka rekodi ya...

MABOSI WAMTAKA BRUNO KUBAKI UNITED

MANCHESTER, Uingereza UONGOZI wa klabu ya Manchester United uko tayari kufanya lolote ili kumbakiza kiungo wake raia wa Ureno,...

CESC FABREGAS KOCHA MPYA CHELSEA?

LONDON, Uingereza KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumkabidhi benchi la ufundi kiungo wao wa zamani raia wa Hispania,...