BERNARDO AWEKA REKODI MPYA MAN CITY

Date:

Share post:

MANCHESTER, Uingereza

KATIKA ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley, kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, ameweka rekodi ya kibabe Ligi Kuu ya England (EPL).

Man City ikiwa ugenini katika Uwanja wa Turf Moor, ilipata bao hilo kupitia kwa Erling Haaland, hivyo kuing’oa kileleni Arsenal baada ya kuizidi mabao ya kufunga.

Matokeo hayo yamewafanya vijana wa Pep Guardiola kushinda mechi tano mfululizo za mashindano mbalimbali walizocheza hivi karibuni.

Bernardo mwenye umri wa miaka 31, anakuwa mchezaji wa Man City aliyeshinda mechi nyingi za EPL (215) katika historia ya klabu hiyo ya jijini Manchester.

Kabla ya mchezo huo dhidi ya Burnley, rekodi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na kiungo wa zamani wa timu hiyo, David Silva.

Kwa msimu huu, Bernardo amecheza mechi 46 za michuano mbalimbali, akidiwa na Nico O’Reilly (48) na Haaland (47) pekee.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

GUARDIOLA AMPONZA KOCHA WA BURNLEY

LONDON, Uingereza KOCHA wa Burnley, Scott Parker, amekalia kuti kavu baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na Manchester...

MABOSI WAMTAKA BRUNO KUBAKI UNITED

MANCHESTER, Uingereza UONGOZI wa klabu ya Manchester United uko tayari kufanya lolote ili kumbakiza kiungo wake raia wa Ureno,...

CESC FABREGAS KOCHA MPYA CHELSEA?

LONDON, Uingereza KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumkabidhi benchi la ufundi kiungo wao wa zamani raia wa Hispania,...

PAPA LEO AKEMEA RUSHWA AKIWA GUINEA

CIUDAD DE LA PAZ, Guinea AKIWA ziarani nchini Guinea ya Ikweta, Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV,...