MANCHESTER, Uingereza
UONGOZI wa klabu ya Manchester United uko tayari kufanya lolote ili kumbakiza kiungo wake raia wa Ureno, Bruno Fernandes.
Kwa wiki za hivi karibuni, zimekuwapo taarifa kuwa huu ni msimu wa mwisho kwa nahodha huyo kukipiga Old Trafford.
Klabu tajiri ya Saudi Arabia, Al-Nassr, inatajwa kutenga kitita cha Pauni milioni 80 kukamilisha usajili wa nyota huyo.
Alikaribia kuondoka wakati wa usajili wa dirisha dogo la Januari, 2026 lakini kocha wa wa wakati huo, Ruben Amorim, alimshawishi kubaki.
Ni wakati ambao Bruno katika moja ya mahojiano yake, alisema baadhi ya vigogo wa klabu hiyo hawataki kumuona akibaki.
Safari hii, viongozi wa Man United wamefanya mazungumzo na Bruno na kumwambia nia yao ni kumbakiza kikosini kwa gharama yoyote.






