GUARDIOLA AMPONZA KOCHA WA BURNLEY

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza

KOCHA wa Burnley, Scott Parker, amekalia kuti kavu baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na Manchester City, matokeo yaliyoishusha Daraja msimu huu wa Ligi Kuu ya England (EPL).

Man City, ambayo sasa iko kileleni mwa msimamo wa EPL kwa tofauti ya mabao, ilipata ushindi huo kwa bao la mapema (dk. 5) la Erling Haaland.

Msimu huu, mabosi wa Burnley walikomaa na Parker, licha ya timu hiyo kushinda mechi moja pekee kati ya 25 za Ligi za hivi karibuni.

Hata hivyo, ripoti zilizopo zinaeleza kuwa mabosi wa klabhu hiyo wanasaka kocha mpya wa kuiongoza timu yao huko Championship.

Akizungumzia hatima yake baada ya Burnley kushuka dareaja, kocha huyo mwenye umri wa miaka 45 amesema: “Ni kawaida kwa kocha kupitia nyakati hizi. Hatukuwa na msimu mzuri.”

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

BERNARDO AWEKA REKODI MPYA MAN CITY

MANCHESTER, Uingereza KATIKA ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley, kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, ameweka rekodi ya...

MABOSI WAMTAKA BRUNO KUBAKI UNITED

MANCHESTER, Uingereza UONGOZI wa klabu ya Manchester United uko tayari kufanya lolote ili kumbakiza kiungo wake raia wa Ureno,...

CESC FABREGAS KOCHA MPYA CHELSEA?

LONDON, Uingereza KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumkabidhi benchi la ufundi kiungo wao wa zamani raia wa Hispania,...

PAPA LEO AKEMEA RUSHWA AKIWA GUINEA

CIUDAD DE LA PAZ, Guinea AKIWA ziarani nchini Guinea ya Ikweta, Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV,...