LONDON, Uingereza
KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumkabidhi benchi la ufundi kiungo wao wa zamani raia wa Hispania, Cesc Fabregas.
Mabosi wa Chelsea wamemfuta kazi Liam Rosenior baada ya timu hiyo kupoteza mechi tano mfululizo za Ligi Kuu ya England (EPL).
Rosenior raia wa England, amekuwa kwenye benchi kwa wiki 15 pekee tangu alipoajiriwa kwa mkataba wa miaka sita na nusu.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 41, aliajiriwa katikati ya msimu huu ili kuziba pengo la Enzo Maresca aliyefukuzwa Januari, 2026.
Fabregas ni miongoni mwa makocha wanaofanya vizuri Ligi Kuu ya Italia (Serie A) akikinoa kikosi cha Como 1907.
Hata hivyo, winga wa zamani wa Chelsea, Florent Malouda, amesema klabu hiyo itakuwa imecheza kamari kumpa kazi Fabregas.
Malouda raia wa Ufaransa, amesema bado kiungo huyo wa zamani wa Arsenal hajaiva vya kutosha kukabidhiwa timu kubwa aina ya Chelsea.






