BILIONI 3 ZAKARABATI SHULE ZA MSINGI

Date:

Share post:

 

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI imetumia shilingi bilioni 3.29 kukarabati na kugharamia shughuli za utawala, michezo, mitihani na posho kwa maafisa elimu kata na walimu wakuu kuanzia mwaka wa fedha 2015/2016 hadi 2019/2020.

Fedha hizo zimetolewa na serikali kupitia mpango wa elimu bila malipo unaotekelezwa na Serikali ya Rais John Pombe Magufuli ambao hadi sasa umezinufaisha pia shule za sekondari 23.

Hayo yameelezwa jana na Kassim Majaliwa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika majukwaa ya kisiasa wilayani Ukerewe ambako amefika akiwa katika mfululizo wa ziara zake nchi nzima za kumnadi mgombea urais wa CCM, Rais John Magufuli.

Majaliwa amesema katika utekelezaji wa mfumo wa uboreshaji wa miundombinu ya shule wa lipa kutokana matokeo (EP4R) ulioanza kutekelezwa 2015 hadi 2020, sh milioni 309 zilitolewa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya madarasa, vyoo na ofisi kwa shule mbalimbali zikiwemo Kalandero, Murutunguru na Kakerege.

Amesema kiasi kingine cha sh milioni 873 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya madarasa, vyoo na maabara kwa shule za sekondari mbalimbali nchini zikiwemo Bukongo, Pius Msekwa, Bwisya, Muruti na Lugongo.

Ziara hiyo ya Majaliwa ilimfikisha katika Kisiwa cha Bwisya kilichoko Kisiwa cha Ukara ambako alitembelea Kituo cha Afya cha Bwisya na kukagua wodi ya wanaume na ya wazazi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

JELA MIAKA 30 KWA KUPATIKANA NA BANGI

MAHAKAMA ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya imemhukumu Brown Frank Mwaitubi (31), mkazi wa Kajunjumele, kifungo cha miaka...

DUTERTE KUPANDISHWA KIZIMBANI ICC

MANILA, Ufilipino JOPO la majaji watatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) limethibitisha kuwa Rais wa zamani wa...

WRIGHT: RICE APEWE BALLON D’OR

LONDON, Uingereza MKONGWE wa Arsenal, Ian Wright, amemtaja Declan Rice kuwa anastahili kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka...

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...