PRETORIA, Afrika Kusini
RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Polisi nchini humo, Jenerali Fannie Masemola.
Jenerali huyo anakuwa kiongozi wa tatu kuchunguzwa kuchunguzwa kwa makosa ya uhalifu akiwa Mkuu wa Polisi.
Hatua ya Rais Ramaphosa ‘kumtumbua’ imetokana na Jenerali Masemola kufunguliwa mashitaka ya ufisadi.
Jenerali huyo mwenye umri wa miaka 62, anahusishwa na mkataba tata wenye thamani ya Dola za Marekani 21.
Baada ya kufikishwa mahakamani, Jenerali Masemola alikana mashitaka hayo yanayomkabili.
“Najua kabisa kuwa sina kosa, hakuna kosa nililofanya lakini lazima sheria zifuate,” amesema.






