MAN CITY YATUA KWA ENZO WA CHELSEA

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza

KLABU ya Manchester City inaangalia uwezekano wa kumsajili kiungo wa Chelsea, Enzo Fernandez, wakati wa usajili wa kiangazi.

Kwa wiki za hivi karibuni, Muargentina huyo amekuwa akihusishwa na mpango wa kuondoka Stamford Bridge.

Man City nayo inamtolea macho Enzo, licha ya kuwapo kwa taarifa zinazodai kuwa inamtaka pia kiungo wa Nottingham Forest, Elliot Anderson.

Kocha wa Man City, Pep Guardiola, anaona Enzo ndiye kiungo sahihi wa kuvaa viatu vya Bernardo Silva atakapoondoka mwishoni mwa msimu huu.

Wakati huo huo, mkataba wa Rodri utafikia ukomo mwaka 2027, ingawa Guardiola anaamini ‘mido’ huyo raia wa Hispania ataongeza mwingine.

Enzo mwenye umri wa miaka 25, bado ana mkataba na Chelsea utakaofikia ukomo mwaka 2032.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...

RAIS RAMAPHOSA ‘AMTUMBUA’ MKUU WA POLISI

PRETORIA, Afrika Kusini RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Polisi nchini humo, Jenerali Fannie...

PAPA AKOSOA MATESO YA WAFUNGWA GUINEA

MALABO, Guinea ya Ikweta KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, ameeleza kutokuridhishwa na namna wafungwa wanavyoishi katika...

LEAO AINGIA RADA ZA UNITED, LIVERPOOL

MILAN, Italia MANCHESTER United na Liverpool zimeingia kwenye ushindani mkali wa kuiwania saini ya winga wa AC Milan, Rafael...