LEAO AINGIA RADA ZA UNITED, LIVERPOOL

Date:

Share post:

MILAN, Italia

MANCHESTER United na Liverpool zimeingia kwenye ushindani mkali wa kuiwania saini ya winga wa AC Milan, Rafael Leao.

Wakati huo huo, Manchester City na Real Madrid nazo zimetajwa kwenye mbio za kumsaka Mreno huyo.

Leao amekuwa kwenye kiwango bora msimu huu, ambapo ameshafunga mabao katika mechi za Ligi Kuu ya Italia (Serie A).

Ripoti zinaeleza kuwa Milan watakuwa tayari kumpiga bei nyota wao huyo endapo watawekewa mezani kitita cha Pauni milioni 60.

Dau hilo linatokana na miaka miwili iliyobaki kwenye mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26.

Gazeti la Daily Mail limedai kuwa Leao hana maelewano mazuri na kocha wa sasa wa Milan, Max Allegri.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...

RAIS RAMAPHOSA ‘AMTUMBUA’ MKUU WA POLISI

PRETORIA, Afrika Kusini RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Polisi nchini humo, Jenerali Fannie...

PAPA AKOSOA MATESO YA WAFUNGWA GUINEA

MALABO, Guinea ya Ikweta KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, ameeleza kutokuridhishwa na namna wafungwa wanavyoishi katika...

MAN CITY YATUA KWA ENZO WA CHELSEA

LONDON, Uingereza KLABU ya Manchester City inaangalia uwezekano wa kumsajili kiungo wa Chelsea, Enzo Fernandez, wakati wa usajili wa...