PAPA AKOSOA MATESO YA WAFUNGWA GUINEA

Date:

Share post:

MALABO, Guinea ya Ikweta

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, ameeleza kutokuridhishwa na namna wafungwa wanavyoishi katika magereza nchini Guinea ya Ikweta.

Papa ameyasema hayo alipotembelea magereza ya nchi hiyo, ambapo aliyakuta kwenye hali mbaya.

Gereza maarufu la Bata alilotembelea Kiongozi huyo wa Vatican limekuwa likinyooshewa vidole na wanaharakati wa haki za binadamu.

Kwa mujibu wa Shirika la Haki za Binadamu la Amnesty International, Gereza hilo ni ‘jehanamu’ ya wakosoaji wa Serikali.

Baadhi ya wafungwa wamenyimwa haki ya kukutana na ndugu zao na hawajulikani kama wako gerezani, kwa mujibu wa Amnesty International.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Waziri wa Sheria wa Guinea ya Ikweta, Reginaldo Biyogo Ndong, si kweli kwamba wafungwa wamekuwa wakiteswa katika gereza hilo.

Akizungumza na wafungwa, Papa Leo amewaambia: “Hamko peke yenu. Familia zenu zinawapenda na zinawasubiri. Watu wengi nje ya kuta za gereza wanawaombea.”

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...

RAIS RAMAPHOSA ‘AMTUMBUA’ MKUU WA POLISI

PRETORIA, Afrika Kusini RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Polisi nchini humo, Jenerali Fannie...

LEAO AINGIA RADA ZA UNITED, LIVERPOOL

MILAN, Italia MANCHESTER United na Liverpool zimeingia kwenye ushindani mkali wa kuiwania saini ya winga wa AC Milan, Rafael...

MAN CITY YATUA KWA ENZO WA CHELSEA

LONDON, Uingereza KLABU ya Manchester City inaangalia uwezekano wa kumsajili kiungo wa Chelsea, Enzo Fernandez, wakati wa usajili wa...