MANILA, Ufilipino
JOPO la majaji watatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) limethibitisha kuwa Rais wa zamani wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, atapandishwa kizimbani.
Duterte anakabiliwa na mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu, hasa kwa operesheni yake ya kupinga dawa za kulevya akiwa Rais kuanzia mwaka 2016 hadi 2022.
ICC inadai kuwa operesheni hiyo ya Duterte ilisababisha vifo vingi tangu alipoianza akiwa Meya hadi alipoingia Ikulu.
Wanaharakati wa haki za binadamu wanaeleza kuwa watu 30,000 walipoteza maisha wakati wa operesheni zake hizo.
Mahakama ya ICC imeeleza kuwa ina ushahidi wa kutosha wa kuendeleza mashitaka dhidi yake.






