WRIGHT: RICE APEWE BALLON D’OR

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza

MKONGWE wa Arsenal, Ian Wright, amemtaja Declan Rice kuwa anastahili kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka ya Ballon d’Or msimu huu.

Wright amesema endapo Arsenal itatwaa mataji ya Ligi Kuu ya England na Ligi ya Mabingwa, basi kiungo huyo atastahili tuzo hiyo.

Lejendari huyo ameyasema hayo katika mahojiano yake na kipindi cha televisheni ya mtandaoni ya ‘Stick to Football’.

“Kama Arsenal itakuwa bingwa wa Ligi Kuu, Declan Rice anapaswa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi,” amesema Wright.

“Na kama Arsenal itakuwa bingwa wa Ligi ya Mabingwa, basi atapaswa kuwa mshindi wa Ballon d’Or.”

Rice (27), alisajiliwa na Arsenal mwaka 2023 akitokea kwa majirani zao wa London, West Ham United, ambapo dili hilo liligharimu Pauni milioni 105.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

DUTERTE KUPANDISHWA KIZIMBANI ICC

MANILA, Ufilipino JOPO la majaji watatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) limethibitisha kuwa Rais wa zamani wa...

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...

RAIS RAMAPHOSA ‘AMTUMBUA’ MKUU WA POLISI

PRETORIA, Afrika Kusini RAIS wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Polisi nchini humo, Jenerali Fannie...

PAPA AKOSOA MATESO YA WAFUNGWA GUINEA

MALABO, Guinea ya Ikweta KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, ameeleza kutokuridhishwa na namna wafungwa wanavyoishi katika...