MKONGWE WA MAN UNITED ATAKA CARRICK APEWE AJIRA

Date:

Share post:

MANCHESTER, Uingereza

LEJENDARI wa Manchester United, Gary Pallister, amesema haoni sababu ya mabosi wa klabu hiyo kutafuta kocha wa msimu ujao wakati Michael Carrick anatosha.

Hata hivyo, Pallister amesema Carrick atapaswa kupewa ajira ya moja kwa moja endapo timu hiyo itamaliza msimu huu ikiwa na tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

Carrick (44), ameiwezesha Man United kufika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL), ikitoka kupata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo mgumu wa ugenini dhidi ya Chelsea.

Lakini, bado Man United imeendelea kuhusishwa na kocha mpya kwa ajili ya msimu ujao, huku Oliver Glasner, Andoni Iraola na Julian Nagelsmann wakitajwa zaidi kwenye kibarua hicho.

“Ni kweli hatuchezi soka la kuvutia lakini tumefanikiwa … Nafikiri (Carrick) anastahili kupewa nafasi,” amesema Pallister.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

GUARDIOLA AMPONZA KOCHA WA BURNLEY

LONDON, Uingereza KOCHA wa Burnley, Scott Parker, amekalia kuti kavu baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na Manchester...

BERNARDO AWEKA REKODI MPYA MAN CITY

MANCHESTER, Uingereza KATIKA ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burnley, kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, ameweka rekodi ya...

MABOSI WAMTAKA BRUNO KUBAKI UNITED

MANCHESTER, Uingereza UONGOZI wa klabu ya Manchester United uko tayari kufanya lolote ili kumbakiza kiungo wake raia wa Ureno,...

CESC FABREGAS KOCHA MPYA CHELSEA?

LONDON, Uingereza KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumkabidhi benchi la ufundi kiungo wao wa zamani raia wa Hispania,...