LONDON, Uingereza
MKONGWE wa Chelsea, Ruud Gullit, amesema changamoto kubwa inayomtesa kocha Liam Rosenior ni timu hiyo kuwa na wachezaji wasio na ukomavu.
Kabla ya kuivaa Brighton katika mchezo wa leo Aprili 21, 2026, Blues walifungwa bao 1-0 na Manchester United.
Matokeo hayo yaliiacha katika nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL).
Endapo mambo hayatokaa sawa, kuna hatari kubwa kwa timu hiyo kukosa tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.
Kwa mtazamo wake, Gullit amesema Chelsea ya sasa haina wachezaji wenye sifa ya uongozi ndani ya uwanja.
Mholanzi huyo ameenda mbali zaidi akisema wachezaji aina ya Luka Modric na Toni Kroos wangekuwa na mchango mkubwa kikosini.
“Najua Chelsea wanataka kushinda, lakini wamejaza makinda kikosini. Unahitaji wakongwe wa kuwafundisha hao vijana, maana kila siku wanarudia makosa yale yale,” amesema.






