LONDON, Uingereza
SHIRIKA la Utangazaji la Uingereza (BBC) limetangaza kupunguza wafanyakazi 2,000 ili kuokoa asilimia 10 ya bajeti yake ya mwaka.
BBC imeeleza kuwa asilimia 10 ya bajeti hiyo ni sawa na Dola milioni 677 kwa kipindi cha miaka miwili ijayo.
Akizungumzia hilo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wake, Rhodri Talfan Davies, amesema, “Najua itaibua taharuki lakini tunataka kuwa wawazi juu ya changamoto iliyopo.”
Davies amesema hatua yao hiyo imetokana na mambo kadhaa, ikiwamo mfumuko wa bei, gharama za leseni, sambamba na hali mbaya ya uchumi duniani.
Mapema mwaka huu, BBC iliweka wazi kuwa inapitia changamoto za kiuchumi, ikieleza nia yake ya kupunguza asilimia 10 ya bajeti kufikia mwaka 2029.
Shirika limethibitisha kuwa utekelezaji wa mpango huo unatarajiwa kuanza rasmi Aprili Mosi, 2027.
Hatua hiyo inakuja wakati aliyekuwa Mtendaji wa Kampuni ya Google, Matt Brittin, akijiandaa kushika nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa BCC mapema mwezi ujao.
Imeandaliwa na Hassan Mwacha






