LAGOS, Nigeria
MAMLAKA nchini Nigeria zimemfutia kesi ya kufadhili vikundi vya kigaidi iliyokuwa ikimkabili Waziri wa Sheria wa zamani, Abubakar Malami.
Malami alifunguliwa mashitaka mwanzoni mwa mwaka huu, akitajwa kuvipa msaada wa fedha vikundi hivyo vya kigaidi.
Msingi wa mashitaka hayo, kwa mujibu wa mamlaka, ulitokana na kitendo cha Waziri huyo kutowashitaki wafadhili wa ugaidi, licha ya majina yao kufikishwa ofisini kwake.
Sasa, kwa mujibu wa mwanasheria wake, Adedayo Adedeji, Malami ameondoshewa mashitaka hayo na kubaki na yake ya kumiliki silaha aina ya bastola bila leseni.
Mashitaka hayo yanamuhusu pia mtoto wake wa kiume, licha ya wote wawili kukana mahakamani.
Imeandaliwa na Hassan Mwasha






