Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, ameongoza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kufanya ziara ya kukagua miradi inayotarajiwa kutembelewa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2026.
Ziara hiyo imefanyika leo Aprili 16, 2026, ikiwa na lengo la kuhakikisha miradi yote iko katika hali nzuri na tayari kwa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru utakaopita mkoani humo.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mhe. Telack amesisitiza umuhimu wa maandalizi ya kina ili kuhakikisha miradi hiyo inaleta tija kwa wananchi na kuendana na malengo ya maendeleo ya serikali.
Kamati hiyo imepanga kufanya ukaguzi katika halmashauri zote za Mkoa wa Lindi ili kujiridhisha na utekelezaji wa miradi hiyo.
Kwa mujibu wa ratiba, Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuingia mkoani Lindi Aprili 27, 2026 kupitia Halmashauri ya Kilwa, ukitokea Halmashauri ya Ruangwa ambako maandalizi ya mapokezi yanaendelea.






