WAZIRI WA FEDHA AKWAA URAIS BENIN

Date:

Share post:

PORTO-NOVO, Benin

NI rasmi sasa aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Benin, Romuald Wadagni, ndiye Rais mpya wa Taifa hilo baada ya ushindi wa asilimia 94 ya kura katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Jumapili ya Aprili 12, 2026.

Hata kabla ya matokeo ya mwisho kutangazwa, mgombea wa upinzani katika kiti cha urais, Paul Hounkpe, alishakubali kushindwa, akisisitiza nia yake ya kutaka Taifa hilo lisigawanyike.

Wadagni anachukua nafasi aliyekuwa bosi wake katika awamu iliyopita, Patrice Talon, ambaye hata hivyo anakosolewa kwa kuvibana mbavu vyama vya upinzani.

Hilo lilithibitika baada ya Chama kikuu cha upinzani, Democrats, kushindwa kusimamisha mgombea katika nafasi ya urais.

Hata hivyo, changamoto kubwa inayomkabili Rais mpya, ambaye atakuwa madarakani hadi mwaka 2033, ni pamoja na kiwango kikubwa cha umasikini kwa raia na rushwa katika taasisi za umma.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

XI JINPING AKUTANA NA SHEIKH MOHAMMED BIN ZAYED KUIMARISHA USHIRIKIANO WA CHINA NA UAE

Beijing, China Rais wa China, Xi Jinping, amekutana na Mwenyekiti wa Abu Dhabi na Rais wa Falme za Kiarabu...

RAIS MWINYI AKAGUA MRADI WA MJI WA AFCON

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea na kukagua maendeleo ya...

TRUMP AFUTA PICHA YAKE AKIJIFANANISHA NA YESU AKIDAI IMETAFSIRIWA VIBAYA

Washington, Marekani Rais wa zamani wa Marekani, Donald J. Trump, ametoa ufafanuzi kufuatia picha aliyochapisha katika mtandao wake wa...

CHELSEA WAMTUPIA JICHO WILLIAM GOMES

London, Uingereza Klabu ya Chelsea imeendelea kuonyesha nia ya dhati ya kumsajili kiungo wa pembeni wa FC Porto, William...