MKONDO WA PILI ROBO FAINALI MABINGWA ULAYA, MBIVU NA MBICHI KUANZA KUJULIKANA LEO

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza
MECHI mbili za marudiano za hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya zitachezwa usiku wa leo, kabla ya zingine (2) kuchezwa kesho.

Leo Aprili 14, Atletico Madrid na Barcelona zitarudiana baada ya Wacatalunya kushinda mabao 2-0 wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Camp Nou. Je, Barca ‘watapindua meza’ wakiwa ugenini?

Mchezo mwingine wa leo ni ule Liverpool dhidi ya PSG utakaochezwa Anfield. Mechi ya kwanza ilichezwa Anfield na PSG kushinda mabao 2-0.

Kesho Aprili 15, 2026, Bayern watakuwa nyumbani kuivaa Real Madrid. Bayern walishinda mabao 2-1 katika mechi ya kwanza wakiwa ugenini Santiago Bernabeu.

Pia, Arsenal watakuwa Emirates kuvaana na Sporting Lisbon baada ya Washika Bunduki hao kushinda bao 1-0 kule Ureno.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

LAGOS, Nigeria WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...