RAIS MWINYI AKAGUA MRADI WA MJI WA AFCON

Date:

Share post:

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa Mji wa AFCON Fumba uliopo Mkoa wa Mjini Magharibi.

Ziara hiyo imefanyika leo Aprili 14, 2026, ambapo Rais Mwinyi aliambatana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Riziki Pembe Juma, pamoja na wadau mbalimbali wa mradi huo.

Katika ukaguzi huo, Rais Mwinyi alipata fursa ya kutembelea na kujionea hatua mbalimbali za ujenzi wa uwanja wa kisasa wa AFCON unaojengwa na kampuni ya ORKUN Group ya Uturuki. Uwanja huo unatarajiwa kutumika katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027, ambayo itaandaliwa kwa ushirikiano wa nchi za Afrika Mashariki za Kenya, Uganda na Tanzania.

Aidha, Rais Mwinyi alikagua pia miundombinu mingine inayotarajiwa kuzunguka uwanja huo, ikiwemo hospitali, barabara, migahawa na maduka makubwa (mall). Miradi hiyo inalenga kuboresha huduma za kijamii na kukuza maendeleo ya mji huo wa kisasa.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

XI JINPING AKUTANA NA SHEIKH MOHAMMED BIN ZAYED KUIMARISHA USHIRIKIANO WA CHINA NA UAE

Beijing, China Rais wa China, Xi Jinping, amekutana na Mwenyekiti wa Abu Dhabi na Rais wa Falme za Kiarabu...

TRUMP AFUTA PICHA YAKE AKIJIFANANISHA NA YESU AKIDAI IMETAFSIRIWA VIBAYA

Washington, Marekani Rais wa zamani wa Marekani, Donald J. Trump, ametoa ufafanuzi kufuatia picha aliyochapisha katika mtandao wake wa...

CHELSEA WAMTUPIA JICHO WILLIAM GOMES

London, Uingereza Klabu ya Chelsea imeendelea kuonyesha nia ya dhati ya kumsajili kiungo wa pembeni wa FC Porto, William...

BEKI NEWCASTLE ASAKWA NA VIGOGO ULAYA

LONDON, Uingereza SAINI ya beki wa kushoto wa Newcastle United, Lewis Hall, inawindwa na klabu kadhaa kubwa za Ulaya,...