KOCHA WA ZAMANI WA UNITED APEWA MIKOBA GHANA

Date:

Share post:

ACCRA, Ghana

ALIYEWAHI kuwa kocha msaidizi wa Manchester United wakati ule wa Alex Ferguson, Carlos Queiroz, amekabidhiwa mikoba ya kuinoa timu ya Taifa ya Ghana ‘Black Stars’ inayojiandaa na fainali za Kombe la Dunia za mwaka huu.

Queiroz (73), anachukua mikoba ya Otto Addo, ambaye aliachia benchi Machi 31, 2026 baada ya Black Stars kupoteza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Austria na Ujerumani.

Kocha huyo anaikuta timu hiyo ikiwa hoi kwani pia ilishindwa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika zilizopita (AFCON 2025).

Anatua kikosini akiwa na uzoefu mkubwa wa kuzinoa timu za taifa, zikiwamo Afrika Kusini, Ureno, Iran, Colombia na Misri.

Katika fainali za Kombe la Dunia zitakazoanza Juni, 2026, Ghana imepangwa Kundi L na itacheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Panama (Juni 17).

Imeandaliwa na Hassan Mwacha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

XI JINPING AKUTANA NA SHEIKH MOHAMMED BIN ZAYED KUIMARISHA USHIRIKIANO WA CHINA NA UAE

Beijing, China Rais wa China, Xi Jinping, amekutana na Mwenyekiti wa Abu Dhabi na Rais wa Falme za Kiarabu...

RAIS MWINYI AKAGUA MRADI WA MJI WA AFCON

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea na kukagua maendeleo ya...

TRUMP AFUTA PICHA YAKE AKIJIFANANISHA NA YESU AKIDAI IMETAFSIRIWA VIBAYA

Washington, Marekani Rais wa zamani wa Marekani, Donald J. Trump, ametoa ufafanuzi kufuatia picha aliyochapisha katika mtandao wake wa...

CHELSEA WAMTUPIA JICHO WILLIAM GOMES

London, Uingereza Klabu ya Chelsea imeendelea kuonyesha nia ya dhati ya kumsajili kiungo wa pembeni wa FC Porto, William...