LONDON, Uingereza
SAINI ya beki wa kushoto wa Newcastle United, Lewis Hall, inawindwa na klabu kadhaa kubwa za Ulaya, zikiwemo za Ligi Kuu ya England (La Liga).
Kwa mujibu wa ripoti, klabu zinazopigana vikumbo kuisaka huduma yake ni Chelsea, Arsenal, Manchester City, Manchester United, Liverpool, Barcelona, na Real Madrid.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 21, ameshacheza mechi 42 akiwa na kikosi hicho cha kocha Eddie Howe tangu kuanza kwa msimu huu.
Taarifa zinaeleza kuwa mabosi wa Newcastle hawana mpango wa kumuuza na badala yake wanahaha kumshawishi aongeze mkataba.
Mkataba wake na Newcastle unaisha mwaka 2029 na endapo klabu hiyo italazimika kumuuza, basi itahitaji si chini ya Pauni milioni 55.
Imeandaliwa na Hassan Mwasha






