LAGOS, Nigeria
VIDEO iliyosambaa katika mitandao ya kijamii imemuonesha kijana aliyetajwa kuwa ni mwanafunzi akiomba kuokolewa, huku watekaji wakishinikiza walipwe kwanza Naira milioni 30 (zaidi ya Sh mil. 57 za Tanzania) ili kumwachia.
Kwa mujibu wa John Arum Azi mkazi wa Kaduna na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Jo, alitekwa na watu wasiojulikana alipokuwa akirejea nyumbani na marafiki zake sita, ambao pia wanashikiliwa.
Taarifa zinaeleza kuwa watekaji walimlazimisha kijana huyo kujirekodi akiomba msaada, na kish kuposti kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook.
Watekaji wamesema wanaahitaji kulipwa Naira milioni 30 na endapo itashindikana, basi watachukua uamuzi wa kumuua.
Kwa miaka kadhaa ya hivi karibuni, maeneo mengi ya Nigeria, hasa Kaskazini, yamekuwa yakikabiliwa na matukio ya utekaji.
Matukio hayo yameshuhudiwa kwa wingi zaidi katika majimbo ya Zamfara, Katsina, Kaduna, Sokoto, Niger na Kogi.
Imeandaliwa na Hassan Mwasha






