USICHUKULIE POA! PATORANKING ALIUZA SUMU YA PANYA MITAANI KABLA YA ‘KUTOBOA’

Date:

Share post:

LAGOS, Nigeria

WAHENGA walisema maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kwamba katika kuishi kwako, si nyakati zote zitakuwa za furaha, hivyo unapaswa kujiandaa na changamoto zinazoweza kujitokeza.

Changamoto ambazo, bila kujali ukubwa wake, hazipaswi kukuvunja na kufanya ukate tamaa, bali kukuimarisha katika kuzifikia ndoto ulizonazo.

Ndicho walichokifanya watu maarufu wengi. Changamoto hazikuwarudisha nyuma, bali walizitumia kama chombo cha usafiri kuzifikia ndoto zao.

PATORANKING

Staa wa muziki wa Afrobeats. Patoranking ni mmoja ya wanamuziki wenye majina na utajiri mkubwa kwa sasa nchini Nigeria.

Kabla ya kuingia kwenye sanaa na kumlipa, nyota huyo alikuwa akijihusisha na biashara ya kuuza dawa za panya huko mitaani.

Patoranking alifichua hilo mwaka 2024, aliposema: “Nikiwaambia kuwa niliowahi kuuza dawa za panya mtaamini?”

BANKY W

Nyota wa muziki nchini Nigeria, ambaye kabla ya kuingia na ‘kutoboa’ kupitia muziki, aliwahi kufanya kazi nyingi za kipato cha chini ili kumudu maisha.

Akiwa Marekani kwa masomo, Banky W, ambaye jina lake halisi ni Olubankole Wellington, aliwahi kujiingiza katika biashara ya kuuza visu majumbani.

Wakati mwingine, pia aliweza kufanya kazi ya kuuza ‘baga’ katika Mgahawa wa McDonald ili tu maisha yaende.

P-SQUARE

Paul na Peter Okoye ni mapacha waliowahi kutikisa soko la muziki barani Afrika kupitia Kundi lao la P-Square. Kabla ya ustaa, maisha yao hayakuwa rahisi.

Paul alikuwa fundi wa umeme, wakati Peter alijikita katika utengenezaji wa feni. Mwaka 2014, Peter alisema: “Nilikuwa fundi wa vifaa vya umeme, zikiwamo feni.

TIMAYA

Huyo naye ni mwamuziki maarufu wa Afrobeat. Kabla ya mafanikio makubwa aliyonayo sasa, Timaya alikuwa mmoja ya vijana waliokuwa wakiuza ndizi mitaani.

Alifichua hilo mwaka 2021, aliposema: “Niliwahi kuuza ndizi na sasa ni tajiri. Niliteseka sana lakini sasa ni tajiri. Asante Mungu.”

MERCY JOHNSON

Bibiye mwenye jina kubwa kwenye kiwanda cha filamu za Nigeria (Hollywood). Kabla ya ustaa alionao, Mercy aliwahi kuwa mfanyakazi wa ndani.

Katika moja ya mahojiano yake, alisema: “Unajua kuwa niliwahi kuwa mfanyakazi wa ndani na kufanya kazi zingine za kipato kidogo ili tu kujikimu?”

Pia, Mercy alifichua alivyowahi kuacha shule kutokana na muda mwingi aliokuwa akitumia kutafuta maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SOMA HIYO! ISRAEL NDIYO WAASISI WA MIKWAJU YA PENALTI

LONDON, Uingereza NI jioni ya Agosti 5, 1970 kwenye Uwanja wa Boothferry Park mjini Hull, Manchester United ikiwa ugenini...

AMEJIPATA! LAMPARD ALIVYOREJEA EPL AKIWEKA REKODI

LONDON, Uingereza IKIWA ni miezi 18 tu imepita tangu alipoajiriwa, Frank Lampard ameiwezesha Coventry City kupanda daraja na kurejea...

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...