BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

Date:

Share post:

CATALUNYA, Hispania
KLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha kuvaa viatu vya Robert Lewandowski.

Lewandowski raia wa Poland, anatarajiwa kuondoka Camp Nou wakati wa usajili wa dirisha kubwa, mwishoni mwa msimu huu wa 2025-26.

Awali, Barcelona walimpiga hesabu straika wa Atletico Madrid, Julian Alvarez, kabla ya kubadili ‘gia angani’ na kuhamia kwa Muriqi.

Muriqi anashika anashika nafasi ya pili katika orodha ya wafungaji msimu huu wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga), akiwa na mabao 21 katika mechi 30.

Kinara wa mbio hizo za kuwania kiatu cha dhahabu ni Kylian Mbappe wa Real Madrid, ambaye hata hivyo amemzidi mabao mawili pekee.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...

NEWCASTLE KUMUUZA MSHAMBULIAJI WA BEI MBAYA

LONDON, UingerezaKLABU ya Newcastle United itampiga bei straika raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Yoane Wissa,...