NEWCASTLE KUMUUZA MSHAMBULIAJI WA BEI MBAYA

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza
KLABU ya Newcastle United itampiga bei straika raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Yoane Wissa, ambaye alisajiliwa kwa ada kubwa ya Pauni milioni 50 akitokea Brentford.

Newcastle walilazimika kufanya usajili huo wa haraka ili kuziba pengo la Alexander Isak aliyekuwa amejiunga na Liverpool.

Hata hivyo, ukiwa ni msimu wake wa kwanza klabuni hapo, Wissa hajaweza kuwa na makali aliyotoka nayo Brentford na sasa mabosi wa Newcastle wanataka kumuuza.

Hata hivyo, kwa kiwango alichonacho sasa, Newcastle inatarajiwa kupata si zaidi ya Pauni milioni 20 endapo itampiga bei mwishoni mwa msimu huu.

Wissa amefunga mabao matatu pekee msimu huu, likiwamo moja la Ligi Kuu ya England na ni chaguo la nne kwa kocha Eddie Howe.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...