NANI KOCHA MPYA WA MADRID MSIMU UJAO?

Date:

Share post:

MADRID, Hispania

ALVARO Arbeloa analiongoza benchi la ufundi la Real Madrid hadi mwishoni mwa msimu huu, kisha atakabidhi mikoba kwa kocha mpya.

 Arbeloa aliajiriwa Januari, 2026 kuchukua nafasi ya Xabi Alonso aliyetimuliwa baada ya mfululizo wa matokeo mabaya.

Je, nani kukabidhiwa kijiti baada ya Arbeloa kumaliza mkataba mwishoni mwa msimu huu?

ANDONI IRAOLA

Baada ya Carlo Ancelotti kuondoka, Iraola alihusishwa na Madrid, kabla ya klabu hiyo ya La Liga kumpa ajira Alonso.

Kwa sasa, Iraola anaiona Bournemouth lakini mkataba wake na klabu hiyo ya England utakwisha mwishoni mwa msimu huu (2025-26).

Iraola ni beki wa zamani wa Athletic Bilbao, akiitumikia timu hiyo ya La Liga kwa miaka 12.

JULIAN NAGELSMANN

Ni kocha wa timu ya Taifa ya Ujerumani na kocha huyo ana umri wa miaka 38 tu. Madrid wanaweza kuvutiwa na uzoefu mkubwa alionao Nagelsmann katika soka la Ulaya. Kwa nyakati tofauti, aliwahi kuzinoa Hoffenheim, RB Leipzig na Bayern Munich.

MAX ALLEGRI

Huu ni msimu wake wa pili akiwa kocha wa vigogo wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A), AC Milan. Mbali ya Milan, Muitalia huyo mwenye umri wa miaka 58 amewahi kupata mafanikio makubwa akiwa na Juventus. Ana mkataba wa mwaka mmoja na Milan, hivyo Madrid watalazimika kuuvunja ili kuinasa huduma yake.

JURGEN KLOPP

Mjerumani huyo amekuwa kwenye rada za Madrid kwa miaka mingi, tangu akiwa Liverpool aliyoiacha mwaka 2024.

Klopp hajawa kwenye kazi ya ukocha tangu wakati huo, na badala yake anasimamia maendeleo ya soka katika klabu zilizo chini ya kampuni ya Red Bull.

Endapo status Madrid, atafanya tena kazi na beki wa pembeni, Trent Alexander-Arnold, aliyekuwa naye Anfield.

MAURICIO POCHETTINO

Hivi karibuni, alihusishwa na Tottenham, kabla ya klabu hiyo ya London kumpa ajira Roberto De Zerbi. Kwa sasa, Muargentina huyo anainoa timu ya Taifa ya Marekani, ikikumbukwa pia aliwahi kufanya kazi na klabu za Tottenham, PSG na Chelsea.

Pochettino mwenye umri wa miaka 53, si mgeni Ligi Kuu ya Hispania kwani aliwahi kuinoa Espanyol aliyotemana nayo mwaka 2012.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...