VITONGOJI 15 VYANUFAIKA NA UMEME WA REA NAMTUMBO

Date:

Share post:

WANANCHI  wa vitongoji 15 katika Jimbo la Namtumbo, mkoani Ruvuma, wameanza kunufaika na huduma ya umeme baada ya kukamilika kwa mradi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Uzinduzi wa huduma hiyo umefanywa na Mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria,Dk. Juma Homera, katika vitongoji vya Mtonya na Mandepwende, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita kusogeza huduma ya nishati kwa wananchi wa vijijini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dk. Homera amesema serikali imejipanga kuhakikisha vitongoji vyote vinaunganishwa na umeme ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

“Mpango  huu unahusisha kuunganisha vitongoji vipya kila mwezi, huku akisisitiza kuwa huduma hiyo itawafikia wananchi wote bila kujali aina ya makazi yao,”amesema Dk Homera

“Lengo la serikali ni kuhakikisha hata nyumba za nyasi zinapata umeme, ili kuboresha maisha ya wananchi na kuongeza fursa za kiuchumi,” amesema Dkt. Homera.

Kwa upande wake, mwakilishi wa REA Deo Nangu, amesema mradi huo umegharimu takribani shilingi bilioni 1.6 hadi kukamilika kwake.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...