Filamu tatu za Tanzania zachomoza kimataifa

Date:

Share post:

Filamu tatu za Tanzania zimepata nafasi kuoneshwa kwenye mtandao wa kimataifa wa kuonyesha filamu wa Netflix.

Hayo yamesemwa na Meneja Mipango na Masoko kutoka Bodi ya Filamu, Goodluck Chuwa, wakati wa ukusanyaji kazi za wasanii wa filamu kwa ajili ya kushiriki kwenye tuzo za filamu Tanzania mwaka 2022.

Amesema kuwa filamu hizo ni Binti, Bahasha pamoja na Nyara, ambazo zimeweza kufanya vizuri kimataifa kutokana na kutengenezwa kwa viwango vyenye ubora.

“Filamu hizo ni sehemu ya kielelezo kwamba sasa soko la filamu zetu limekua na wasanii wetu kutoa kazi ambazo zina ubora mkubwa hadi kushindanishwa kimataifa,”amesema Chuwa.

Naye Ofisa Utamaduni Mkoa wa Tanga, Emmanuel Makene amewataka wasanii wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye tuzo hizo.

Jumla ya vipengele 31 vinashindaniwa katika tuzo hizo, huku mwisho wa kuwasilisha kazi za wasanii ikiwa ni Oktoba 30 mwaka huu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...