TANGA
MWANAFUNZI wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Chief Mang’enya iliyopo Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, Abdallah Msenga amefariki dunia baada ya kugongana kichwa na mwanafunzi mwanzeke, Abdallah Bakari.
Tukio hilo limetokea wakati wa mechi ya ligi ya ndani ya shule hiyo iliyokuwa ikizikutanisha timu za wanafunzi wa kidato cha nne mkondo wa AB na CB.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almanus Muchunguzi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema limetoa Februari 22, 2026 katika viwanja vya shule hiyo.
Kamanda Muchunguzi amesema mwanafunzi huyo alikuwa akigombea mpira na mchezaji mwenzake wa timu pinzani, Abdallah Bakari ndipo walipogongana vichwa na kusababisha marehemu kuanguka chini.
“Waligongana na marehemu aligongwa sehemu ya kushoto na kukimbizwa katika hospitali teule ya Wilaya ya Muheza ingawa alipoteza maisha wakati akipatiwa matibabu,” amesema Kamanda Muchunguzi,
