KOCHA ALIYEKUFUZWA YANGA, AOMBA KURUDI

Date:

Share post:

KOCHA mkuu wa zamani wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet, ni miongoni mwa makocha watano walioomba kibarua cha kuifundisha timu hiyo, kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano mingine.

Saintfiet aliwahi kuifundisha Yanga kwa siku 80 kabla ya kufukuzwa Julai 4, 2012, baada ya kufungwa mabao 3-0 na timu ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.

Kabla ya kutimuliwa kwake, Saintfiet alianza msimu vibaya baada ya kupata suluhu na Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya, licha ya kuiwezesha Yanga kutwaa ubingwa wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu Kombe la Kagame yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Kwa sasa, Santifiet ambaye ni kocha wa timu ya Taifa ya Mali, imeelezwa kwamba kocha huyo amewasilisha wasifu wake (CV), akiomba kurithi mikoba ya Miloud Hamdi aliyeachana na klabu hiyo baada ya kumalizika kwa msimu wa 2024/2025 wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Chanzo chetu kiliwataja makocha wengine waliojitokeza kuomba kurithi mikoba ya Hamdi ni pamoja na Rulani Mokwene wa Mamelodi Sundowan ya Afrika Kusini na julien Chevalier wa Asec ya Ivory Coast

Hata hivyo, Panorama ilimtafuta Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe, kwa lengo la kujua uweli kuhusu hilo, lakini simu yake iliita bila majibu,

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

BBC KUPUNGUZA WAFANYAKAZI 2,000

LONDON, Uingereza SHIRIKA la Utangazaji la Uingereza (BBC) limetangaza kupunguza wafanyakazi 2,000 ili kuokoa asilimia 10 ya bajeti yake...

MATUMAINI YAKONEKANA BAADA YA MAREKANI NA IRAN KUPATANISWA NA PAKISTAN

Maafisa wa Pakistan wanatarajia kupatikana kwa “mafaanikio makubwa” katika mazungumzo yanayoendelea kati ya Iran na Marekani kuhusu mpango...

IRAN YAKAMATA WAPELELEZI WA ISRAEL

TEHRAN, IranIMERIPOTIWA kuwa Iran inawashikilia watu wanne waliowataja kuwa ni wapelelezi wa Israel. Taarifa hiyo inakuja wakati huu wawakilisi...

DANGOTE, TRUMP WATAJWA WATU WENYE USHAWISHI ZAIDI DUNIANI

WASHINGTON DC, MarekaniMFANYABIASHARA maarufu Afrika, Aliko Dangote, ni miongoni mwa watu 100 wenye ushawishi duniani, kwa mujibu wa...