MAZINGAOMBWE YA KAMPUNI YA PARAMOUNT

Date:

Share post:

 

Ufuta


NA MWANDISHI WETU

KAMPUNI ya Paramount Limited ya mkoani Dar es Salaam inayojihusisha na biashara ya mazao mbalimbali inadaiwa kuendesha shughuli zake kinyemela ndani ya eneo la mamlaka ya maeneo maalumu ya uzalishaji kwa mazao ya nje (EPZ)

Sambamba na hilo kampuni hiyo inadaiwa kuajiri raia wa kigeni wasiokuwa na vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini, kukwepa kulipa kodi na pia kutotekeleza matakwa ya sheria za ajira.

Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya ofisi hizo zimedai kuwa, kampuni hiyo inaendesha shughuli zake za biashara ndani ya jengo linalomilikiwa na kampuni nyingine ambayo jina lake tunalihifadhi kwa sasa

Inadaiwa Paramount imekuwa ikinunua mazao na kuuza nje ya nchi, kuajiri raia wa kigeni wasiokuwa na vibali vya kuishi wala kufanya kazi nchini na kufunga mitambo ya kusafishia mazao bila ya kuwa na ofisi.

Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo aliyezungumza na waandishi wa habari (jina tunalihifadhi) amesema kuwa shughuli zote za kibiashara za kampuni hiyo zinafanywa ndani ya eneo la kampuni nyingine.

“Hawa wahindi ni watu wa ajabu sana. Huyu sisi ametuajiri lakini kwanza hatuna mikataba ya kazi, hatuna pensheni ya aina yoyote ile yaani kiufupi hafuati taratibu zote za ajira za hapa nchini.

“Hapa ndani, hizi siyo ofisi zake, hii kampuni haina ofisi ujue, hizi ni ofisi za kampuni nyingine lakini jamaa huyu wa Paranount amejificha humu, anafanya biashara lakini halipi kodi wala nini kwa sababu hizi siyo ofisi zake.


“Sasa humu amefunga mashine za kusafishia ufuta, ufuta una vumbi sana kuusafisha hivyo wafanyakazi wanatakiwa kuwa na vifaa vya kujikinga na hilo vumbi kwa ajili ya afya zao lakini hawa hawana kifaa chochote, vumbi lote linawaingia wanaishia kuumwa vifua na hana huruma, ukiugua anakufukuza kazi.

“Hakuna mamlaka za Serikali zinazojua ofisi za hii kampuni zilipo kwa hiyo siyo rahisi kuzifuatilia, hizo mashine hata TRA hawajui kama zimefungwa humu na zinafanya kazi ya kusafisha ufuta.

“Jamaa wa hii kampuni wanajifanya wawekezaji lakini wana madudu mengi sana na wanafanya wanavyotaka kwa sababu Serikali haijui lolote kuhusu ofisi zao zilipo maana wamejificha kwenye kampuni nyingine,” alisema mtoa taarifa.

Alipoulizwa mkurugenzi wa Kampuni ya Paramount aliyetambulika kwa jina moja la Dawal, kuhusu madai hayo alisema anayeweza kuyazungumzia ni msemaji wake ambaye alitoa namba zake za simu ili atafutwe.

Alipotafutwa msemaji huyo ambaye hata hivyo imebainika ni mmoja wa wamiliki wa jengo ambalo Paramount inaendesha shughuli zake kwa uficho, alisema hayuko katika nafasi nzuri ya kuzungumza hivyo atafutwe baadaye na alipotafutwa baadaye kama alivyoomba alisema aulizwe Dawal mwenyewe azungumzie matatizo yake.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

LONDON, Uingereza BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...