MKENYA WA FARMER’S CHOICE AKIRI KUNUNUA NYAMA VINGUNGUTI

Date:

Share post:

Nyama zinazouzwa machinjio ya Vingunguti

 

NA MWANDISHI WETU

MWAKILISHI wa Kampuni ya Farmer’s Choice ya Kenya, Coroline Manka aliyeletwa nchini kusimamia bidhaa za nyama zinazozalishwa na kampuni hiyo amekiri kuwa Kampuni ya Bright Choice inanunua nyama katika machinjio ya Vingunguti.

Akizungumza leo na Tanzania PANORAMA Blog kuhusu tuhuma inazoelekezewa Kampuni ya Bright Choice Limited kuwa imekuwa ikighushi nembo za Kampuni ya Farmer’s Choice Limited na kuziweka katika bidhaa zake, alisema anachofahamu yeye, nyama inayonunuliwa Vingunguti ndiyo inayotengenezwa na kuuzwa na Kampuni ya Bright Choice.

Alizitaja bidhaa za nyama zinazotengenezwa na Bright Choice kuwa ni ‘beef fillet na beef mince,’ na kwamba soko lake kubwa liko mkoani Arusha.

Akizungumza kuhusu majukumu yake ndani ya kampuni hiyo alisema ni kweli kwamba aliletwa hapa nchini na Kampuni ya Farmer’s Choice kama mwakilishi wake na pia alikiri kuwa alipofika hapa nchini aliajiriwa na Kampuni ya Bright Choice kwa majukumu tofauti na aliyopewa na Farmer’s Choice ya Kenya.

Hata hivyo, Manka alikataa kuzungumzia tuhuma za Kampuni ya Bright Choice kutengeneza bidhaa bandia za Farmer’s Choice na kutaka atafutwe Mkurugenzi wa Bright Choice kuzungumzia suala hilo.

Baadaye, mmoja wa wakugenzi wa Kampuni ya Bright Choice, Jacob Mlingi, aliipigia simu Tanzania PANORAMA Blog akiomba miadi ya kukutana na mwandishi kwa mazungumzo lakini alipoambiwa atoe ufafanuzi wa kile anachokifahamu kuhusu tuhuma inazoelekezewa Bright Choice alikataa kusema chochote.

Tanzania PANORAMA Blog inaendelea kufuatilia sakata hili.

 

 

 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU ZIARA YA PAPA LEO BARANI AFRIKA

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, yuko barani Afrika kwa ziara ya siku 10 katika mataifa...

MATESO WANAYOPITIA WATOTO KATIKA MACHAFUKO YA SUDAN

DARFUR, Sudan "HALI ya watoto nchini Sudan inazidi kuwa mbaya kila baada ya saa moja." Hiyo ni kauli ya...

IRAN: TUKO TAYARI KWA VITA MAZUNGUMZO YAKISHINDIKANA

TEHRAN, IranSPIKA wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema nchi yake itakuwa tayari kwa mbinu mpya za...

RAIS WA BRAZIL AMVAA TRUMP, AITAKA AFRIKA KUSINI KUMPUUZA

BERLIN, Ujerumani RAIS wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva, amesema Donald Trump hana mamlaka ya kumzuia Cyril Ramaphosa...