MBOWE ATOKA HOSPITALINI

Date:

Share post:

MACHI 6, 2018
Mbowe

MOSHI 
MWENYEKITI  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, jana usiku aliruhusiwa kutoka hospitalini alikokuwa akitibiwa na kurejea nyumbani.
Mbowe alilazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, baada ya kujisikia vibaya ghafla ikiwa ni saa chache kabla ya kuripoti polisi, yeye na viongozi wenzake sita wa Chadema kama walivyotakiwa na polisi.
Taarifa za kitabibu zilizopatikana jana, zilieleza kuwa alipofikishwa hospitali hapo alikuwa akilalamika kusumbuliwa na maumivu ya kichwa na baada ya kufanyiwa uchunguzi aligundulika kuwa anasumbuliwa na uchovu.
Akiwa hospitalini hapo aliwekewa mashine ya oksijeni kwa ajili ya kumsadia kupumua.
Afisa Uhusiano wa KCMC , Gabriel Chisseo amekaririwa akieleza kuwa Mbowe aliruhusiwa na madaktari kutoka hospitali muda wa 1:30 usiku baada ya kujiridhisha kwamba hali yake inaendelea vizuri.
Katibu wa Chadema wa Mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema naye alizungumzia kuimarika kwa afya ya Mbowe lakini alisema hajui alipo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

LONDON, Uingereza BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...