RORYA YAMWAGIWA BILIONI 5.8 ZA ELIMU BILA MALIPO

Date:

Share post:

 

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI imetoa shilingi bilioni 5.8 kwa shule 151 za Wilaya ya Rorya mkoani Mara kwa ajili ya kugharamia mpango wa elimu bila malipo unaotekelezwa na serikali ya awamu ya tano tangu ilipoingia madarani mwaka 2015.

Fedha hizi zimenufaisha shule za sekondari 31 na za msingj 120.

Akizungumza na wananchi wa Shirati kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa mpira Obwere, Kata ya Mkoma, Wilaya ya Rorya, Mkoa wa Mara, Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa alisema sh. bilioni 3.3 zilitolewa na serikali ya Rais John Pombe Magufuli kwa ajili ya shule za msingi 120.

Majaliwa alisema fedha hizo zilitolewa kwa ajili ya ukarabati, masuala ya utawala, michezo, mitihani na posho kwa maafisa elimu kata na walimu wakuu.

Alisema kwa shule za sekondar 31, serikali ilitoa sh bilioni 2.5 kwa ajili ya fidia ya ada, chakula kwa shule za bweni na posho ya madaraka kwa wakuu wa shule.

Majaliwa alisema serikali kupitia mpango wa lipa kutokana na matokeo (EP4R)  pia ilitoa sh bilioni 1.2 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya shule ambayo ni pamoja na ukamilishaji wa miundombinu ya madarasa, vyoo na nyumba za walimu kwa shule za msingi.

Alizitaja baadhi ya shule za msingi zilizonufaika na mpango huo kuwa ni Mori, Nyanduga, Buchuri, Kondo, Saye, Masonga, Kyaro, Kitembe, Bubombi, Oliyo B, Dagopa, Nyabi, Ratia, Kotwo, Muchirobi, Manyara, Ochuna na Nuamaguku.

” Kwa upande wa shule za sekondari zimetumika sh milioni 777.8 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya shule ikiwemo maabara, madarasa, mabweni na vyoo kwa shule za Bukama, Mirage, Ngasaro, Nyamunga, Buturi, Goribe, Nyathorogo, Nyamtinga na Waningo.

Waziri Mkuu Majaliwa yupo Mkoa wa Mara akifanya kampeni za kumuombea kura mgombea urais wa CCM, Rais John Pombe Magufuli na aliitumia fursa ya mkutano huo kuwaombea kura mgombea ubunge wa Jumbo la Rorya, Jafari Chege, mgombea udiwani wa Kata ya Mkoma, Ayoi Mussa Sonde na madiwani wengine wa wilaya hiyo.

 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

JELA MIAKA 30 KWA KUPATIKANA NA BANGI

MAHAKAMA ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya imemhukumu Brown Frank Mwaitubi (31), mkazi wa Kajunjumele, kifungo cha miaka...

DUTERTE KUPANDISHWA KIZIMBANI ICC

MANILA, Ufilipino JOPO la majaji watatu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) limethibitisha kuwa Rais wa zamani wa...

WRIGHT: RICE APEWE BALLON D’OR

LONDON, Uingereza MKONGWE wa Arsenal, Ian Wright, amemtaja Declan Rice kuwa anastahili kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka...

ISRAEL, LEBANON ZAONGEZA WIKI TATU ZA KUSITISHA VITA

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Israel na Lebanon zimekubaliana kuongeza wiki tatu za kusitisha mapigano. Wakati...