![]() |
Kamanda Bukombe |
NA MWANDISHI WETU
ALIYEKUWA Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni (RPC), Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Edward Bukombe, amehamishwa kituo chake cha kazi na kupelekwa makao makuu.
Taarifa zilizoifikia Tanzania PANORAMA Blog kutoka vyanzo vyake vya habari zimeeleza kuwa Kamanda Bukombe sasa anakwenda kuongoza kitengo cha picha na matukio na kwamba uhamisho huo ni wa kawaida.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, nafasi ya Kamanda Bukombe imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ramadhani Kingai ambaye katika mahojiano yake leo na Tanzania PANORAMA Blog amethibitisha kurithi wadhfa huo akitokea mkoani Arusha.